Psalms 3:1-6
Sala Ya Asubuhi Ya Kuomba Msaada
Zaburi Ya Daudi Alipomkimbia Mwanawe Absalomu.
1 aEe Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi!
Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
2 bWengi wanasema juu yangu,
“Mungu hatamwokoa.”
3 cLakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote;
umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
4 dNinamlilia Bwana kwa sauti kuu,
naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
5 eNinajilaza na kupata usingizi;
naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
6 fSitaogopa makumi elfu ya adui,
wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
Copyright information for
SwhKC